Sasa timu hiyo ya kocha Ahmed Hassan ‘Mido’ imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 5-0 baada ya sare ya 0-0 katika mchezo wa kwanza mjini Kitwe wiki iliyopita.
Jana Ahmed Tawfik alifunga bao la kwanza dakika ya 20 kabla ya Momen Zakrya kufunga la pili na Zamalek walikwenda kupumzika wakiwa wanaongoza 2-0.
![]() |
Wachezaji wa Zamalek wakishangilia ushindi wao jana |
Kipindi cha pili Omar Gaber akafunga la tatu, Hazem Emam la nne na Ahmed Gafer la tano.
Zamalek sasa imeungana na Al Ahli Benghazi ya Libya, TP Mazembe ya DRC, CS Sfaxien ya Tunisia,
Vita Club ya Kongo, Esperance ya Tunisia, El Hilal ya Sudan na Entente Setif ya Algeria.
Post a Comment